Korea Kaskazini imefanya jaribio la kombora jipya la masafa marefu linaloweza kupiga sehemu kubwa ya Japan, vyombo vya habari vya serikali vimesema.
Jaribio lililofanywa mwishoni mwa wiki lilishuhudia makombora yakisafiri hadi umbali wa km1,500 (930 maili),kulingana na KCNA.
Jaribio hilo halikiuki maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa - lakini yalisababisha vikwazo vikali kwa Korea Kaskazini hapo zamani.
Jaribio la kombora la baharini linatoa "umuhimu wa kimkakati wa kumiliki kigingi kingine ni katika kuhakikisha usalama wa nchi yetu na nguvu za kijeshi dhidi ya vikosi vyenye uhasama," KCNA ilisema.
Jeshi la Marekani limesema kuwa jaribio hilo lilionesha "Korea Kaskazini inaendelea kuzingatia kukuza programu yake ya kijeshi na vitisho ambavyo vinapeleka kwa majirani zake na jamii ya kimataifa".
Iliongeza kuwa inazingatia kwa dhati nia yake ya kutetea washirika wake Korea Kusini na Japan.
#ChanzoBBCSwahili