Star Tv

Rais wa zamani wa Afghanistan Ashraf Ghani ameomba msamaha kwa watu wa Afghanistan baada ya kukimbilia katika nchi za Falme za Kiarabu.

Rais Ghan amewaambia raia wake kuwa ilimbidi afanye maamuzi magumu; "Kuondoka Kabul ulikuwa uamuzi mgumu zaidi maishani mwangu," amesema, akiongeza kuwa anajuta kwamba "hakuweza kumaliza hilo kwa njia tofauti."

Bwana Ghani aliondoka ghafla nchini Afghanistan wakati wanamgambo wa Taliban walipokuwa wakiendelea kuingia kwenye mji mkuu mnamo Agosti 15.

Alisema hakuwa na nia ya kuwaacha watu wake lakini "ilikuwa ndio njia pekee iliyosalia."

Katika taarifa iliyoshirikishwa kwenye mtandao wa Twitter siku ya Jumatano, Bw. Ghani alisema hakuwa na njia nyingine yoyote zaidi ya kuondoka nchini humo ili kuepusha kuenea kwa ghasia.

"Niliondoka kwa kushawishiwa na usalama wa ikulu, ulionishauri kuwa kuendelea kuwepo kulihatarisha kutokea kwa mapigano mitaani na katika barabara za mji kama ilivyotokea wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka ya 1990,"- aliandika, akiongeza kuwa alifanya hivyo "kuokoa mji wa Kabul na raia wake Milioni sita".

Alisema alikuwa amejitolea kwa kipindi cha miaka 20 kusaidia Afghanistan kuwa "nchi ya kidemokrasia, mafanikio na huru."

Bwana Ghani ameongeza kuwa alikuwa na "masikitiko makubwa" kwamba "muda wangu mwenyewe uliishia kwa majuto kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wangu."

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.