Star Tv

Jeshi la Nigeria limesema wanajeshi kumi na moja wameuawa katika shambulio lilifanyika katika jimbo la kati la Benue wakati wa operesheni ya kawaida.

Haya yanajiri wakati hali ya usalama ikiendelea kuzorota kote Nigeria na vikundi mbalimbali vyenye silaha vikianzisha vurugu.

Jeshi la Nigeria linasema kwamba askari hao, hapo awali walitangazwa kutoweka baada ya kuviziwa na watu wenye silaha.

Timu ya kuwatafuta na uokoaji baadaye iliwakuta wamefa siku ya Alhamisi katika eneo la Konshisha katika jimbo hilo.

Msemaji wa jeshi la Nigeria ameiambia BBC kwamba baadhi ya miili hiyo iliteketezwa. Alifafanua shambulio hilo kama uhalifu mbaya. 

Kumekuwa na ripoti kwamba wanajeshi wamewafyatulia risasi kiholela raia kadhaa kujibu shambulio dhidi ya wanajeshi.

Jeshi la Nigeria limekanusha madai hayo. Bado haijafahamika ni nani aliyewauwa wanausalama na kwanini.

Lakini kama sehemu nyingi za Nigeria, jimbo la Benue limekuwa likikabiliwa na ghasia za kikabila, mapigano kati ya wafugaji na wakulima na shughuli za magenge ya wahalifu wenye silaha.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.