Star Tv

Marekani imebadili uamuzi wa kulegeza kwa muda, vikwazo dhidi ya Bilionea wa Israel Dan Gertler, anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi unaohusisaha biashara ya madini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Hatua hiyo ya hivi punde inabatilisha uamuzi uliotolewa siku za mwisho za utawala wa rais wa zamani wa Marekani Donald Trump.

Mwaka 2017 na 2018, hazina ya Marekani iliweka vikwazo dhidi ya Bw. Gertler ambayo ilimzuia kufanya biashara na raia wa nchi hiyo na taasisi zake, hatua ambayo ilimzuia kupata huduma za benki za kimataifa.

Ilimtuhumu kwa ufisadi na ukiukaji wa maadili katika sekta ya madini na kutumia ushirikiano wake na rais wa zamani wa DR Congo, Joseph Kabila kupata mikataba ya kibiashara.

Hata hivyo, Bw. Gertler amekana kufanya makosa yoyote.

Utawala wa Trump ulikuwa umemuondolea vikwazo Bw. Gertler kwa kipindi cha mwaka mmoja hadi Januari 31, mwaka 2022, kuendelea kufanya biashara na kampuni za Marekani.

Chanzo:BBC Swahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.