Star Tv

Dunia inaadhimisha leo siku ya kimataifa ya Wanawake, kauli mbiu ya mwaka huu ikiwa ''Wanawake katika uongozi: Kufikia mustakabali ulio sawa katika dunia yenye janga la COVID-19.''

Katika taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres sambamba na maadhimisho haya, kiongozi huyo amehimiza kuwashirikisha kikamilifu wanawake katika sekta zote za maendeleo.

Aidha,Mbali na kutoa msisitizo huo, Katibu Mkuu amesema anasikitishwa kuona kuwa hadi sasa uwakilishi wa wanawake katika nafasi za kuchukua maamuzi bado ni wa kiwango cha chini.

Ametoa mfano kuwa wanawake ni viongozi wa serikali za nchi 22 tu duniani, ikiwa asilimia 24.9 tu ya viongozi wote katika wadhifa wa ngazi hiyo.

Aidha, Kaulimbiu ya mwaka huu inahimiza nafasi sawa kwa kizazi cha sasa, ili kufanikisha usawa wa kijinsia mnamo miaka ijayo.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.