Star Tv

Wafanyakazi zaidi katika ikulu ya Marekani wamepatikana na virusi vya corona.

 Wafanyakazi hao wamegundulika ikiwa tu ni siku chache tu baada ya rais Donald Trump kulazwa hospitalini baada ya kupatikana na virusi hivyo.

Baadhi ya wafanyakazi wa hivi punde kuambukizwa ni pamoja na, mshauri mkuu katika ikulu ya White House, Stephen Miller, ambaye amekuwa karantini kwa siku chache zilizopita, na afisa mkuu katika jeshi.

Aidha, kwa sasa, Jenerali wa juu wa Marekani Mark Milley na viongozi wengine wa kijeshi wamejitenga baada ya Charles Ray kupatikana na maambukizi hayo.

Wakati hayo yakijiri, kati ya maafisa waliohudhuria mikutano na Charles Ray wiki iliyopita ambao kwa sasa wako karantini, hakuna mmoja wao ambaye amethibitika kuwa na maambukizi hayo au hata kuonesha dalili zozote za ugonjwa huo

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.