Wafanyakazi zaidi katika ikulu ya Marekani wamepatikana na virusi vya corona.
Wafanyakazi hao wamegundulika ikiwa tu ni siku chache tu baada ya rais Donald Trump kulazwa hospitalini baada ya kupatikana na virusi hivyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa hivi punde kuambukizwa ni pamoja na, mshauri mkuu katika ikulu ya White House, Stephen Miller, ambaye amekuwa karantini kwa siku chache zilizopita, na afisa mkuu katika jeshi.
Aidha, kwa sasa, Jenerali wa juu wa Marekani Mark Milley na viongozi wengine wa kijeshi wamejitenga baada ya Charles Ray kupatikana na maambukizi hayo.
Wakati hayo yakijiri, kati ya maafisa waliohudhuria mikutano na Charles Ray wiki iliyopita ambao kwa sasa wako karantini, hakuna mmoja wao ambaye amethibitika kuwa na maambukizi hayo au hata kuonesha dalili zozote za ugonjwa huo