Star Tv

Hatua iliyotangazwa wiki iliyopita na Ethiopia ya kuanza kwa zoezi la kujaza bwawa kubwa la kuzalisha umeme la Renaissance kwenye Mto Nile linaendelea kuzua mvutano na nchi jirani zilizo na mto huo.

Kazi katika mradi wa bwawa la maji la kuzalisha umeme huko Ethiopia imeshika kasi, huku jaribio la kuutatua mgogoro wa Ethiopia na nchi jirani zinazopakana na mto Nile zikiendelea.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres Jumanne wiki hii aliziataka Ethiopia, Sudani na Misri kuwa na "uvumilivu" katika juhudi zao za kufikia makubaliano, ambapo mazungumzo ya Washington yalisitishwa tangu mwezi Februari.

Katikati ya mzozo huo ni mpango wa kujaza bwawa hilo kuu, Ethiopia inataka kutekeleza mpango huo kwa kipindi cha miaka sita, Misri ikipendekeza muda wa miaka kumi ikihofu mradi huo utafanya Ethiopia kudhibiti maji ya mto Nile.

Mradi huu unaotarajiwa kuanza kuzalisha umeme kuanzia mwaka 2022 utagharimu dola bilioni nne za kimarekani, Ni mradi mkubwa lakini umesababisha pia mgogoro wa kidiplomasia kati ya Misri na Sudan kwani nao wanategemea maji ya mto Nile.

Bwawa hilo linalojengwa Kaskazini mwa Ethiopia, litakuwa kituo kikubwa kabisa cha kuzalisha umeme barani Afrika.

Lakini Misri, ambayo inategemea maji ya mto Nile kwa 80%, ina hofu kuwa bwawa hilo litaathiri mfumo wa usambazaji maji ambao nao una changamoto kadhaa.
Mara baada ya kukamilika, bwawa hilo litakalokuwa na uwezo wa megawatt 6000 litakalogharimu pauni bilioni tatu, lakini ujenzi huo umeathiriwa na ucheleweshaji na haijafahamika kama litaanza kufanya kazi baada ya muda wa mwisho uliowekwa na serikali mwaka 2021.

Bwawa hilo lenye urefu wa mita 145, karibu kilometa 2 linatarajiwa kuwa chanzo kikubwa cha kuzalisha umeme nchini Ethiopia.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.