Star Tv

Maaskofu wa kanisa Katoliki nchini Msumbiji wameishambulia serikali kutokana na kile walichosema ni kushindwa kwa serikali hiyo kuzuwia wapiganaji wa itikadi kali ya Kiislamu kuvuruga eneo la kaskazini mwa nchi hiyo, wakidai mamia ya raia wamepoteza maisha.

Askofu wa jimbo la Pemba na rais wa tume ya haki na amani ya baraza la maaskofu, Dom Luiz Fernandes, amewashutumu maafisa wa kitaifa na jumuiya ya kimataifa kwa kutofanya vya kutosha kuzuwia wimbi la mashambulizi ambalo amelifananisha na kimbunga. Matamshi yake yamekuja wiki kadhaa kabla ya ziara ya mwezi Septemba nchini Msumbiji itakayofanywa na kiongozi wa kanisa Katoliki Papa Francis kama sehemu ya ziara ya mataifa ya Afrika ambayo pia itamfikisha Madagascar na Mauritius.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.