Star Tv

Idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na ajali ya boti katika Ziwa Kivu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imefikia 40, kufuatia kupatikana kwa maiti nyengine 27 jana Jumamosi.

Waziri wa mambo ya ndani, Basile Olongo, ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba miili hiyo ilipatikana mpakani mwa kingo za mashariki za ziwa hilo upande wa nchi jirani ya Rwanda. Boti hiyo ilipinduka mwanzoni mwa wiki hii ikiwa imebeba watu takribani 200 na hadi sasa watu zaidi ya 100 hawajajulikana walipo. Rais Felix Tshisekedi aliitangaza Ijumaa kuwa siku ya maombolezo ya kitaifa. Ajali za vyombo vya majini zimekuwa jambo la kawaida katika mataifa mengi ya Maziwa Makuu, ambako vyombo kadhaa vya usafiri ni vikongwe na hujaza abiria kupita kiwango, huku vikiwa havina huduma za uokozi.

CHANZO: IDHAA YA KISWAHILI DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.