Star Tv

Msumbiji: Misaada yaanza kuwafikia waliokumbwa na maafa ya kimbunga Idai

Watu walionusurika maafa yaliyosababishwa na kimbunga Idai kilichokumba eneo la Kusini mwa Afrika wameanza kupatiwa misaada ya haraka ya dawa, chakula na mahema.

Kwa mujibu wa taarifa mafuriko yameanza kupungua. Maalfu ya watu waliokuwa wamekwama wiki iliyopita sasa wanapelekwa kwenye sehemu zenye usalama zaidi. Hata hivyo Shirika la Msalaba Mwekundu limetahadharisha juu ya hatari ya kuzuka maradhi ya kuambukiza. Kimbunga Idai kiliukumba mwambao wa Msumbiji na sehemu za Mashariki mwa Zimbabwe na kusabaisha vifo vya watu 700 katika nchi hizo mbili. Na nchini Malawi watu wapatao 56 walikufa kutokana na kimbunga hicho.

Chanzo: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.