Star Tv
Takriban miaka mitano baada ya kujitoa katika jumuiya ya madola leo Gambia inajiunga upya. Sherehe inafanyika leo Alhamisi katika makao makuu ya jumuiya hiyo mjini London kuidhinisha kurudi kwa nchi hiyo kama taifa mwanachama wa jumuiya ya madola. Mnamo Februari 2017, rais mpya aliyechaguliwa Adama Barrow aliomba nafasi ya taifa lake kurudi kuwa mwanachama, na mwezi Desemba bunge nchini humo liliidhinisha ombi hilo la kurudi katika kundi hilo linalojumuisha mataifa yaliokuwa chini ya ukoloni wa Uingereza. Gambia ilijiondoa katika jumuiya hiyo mnamo Octoba 2013. Rais wa zamani Yahya Jammeh aliishutumu jumuiya hiyo kwa kuwa anachokitaja "taasisi ya ukoloni mambo leo". Aliishutumu Uingereza kwa kuwaunga mkono wapinzani wake wa kisiasa. Yahya Jammeh alilitawala taifa hilo dogo la Afrika magharibi kwa miaka 22. Alishindwa katika uchaguzi mkuu mnamo Desemba 2016 lakini akajaribu kufuta matokeo ya uchaguzi huo. Ilichukua wiki kadhaa za majadiliano na tishio la jeshi kuingilia kati kumlazimisha aachilie madaraka. Baada ya Afrika kusini, Pakistan na Fiji, sasa Gambia inakuwa nchi ya nne kurudi katika jumuiya ya madola. Afrika kusini ilitangaza kujitoa katika jumuiya hiyo mnamo Mei mwaka 1961 baada ya kupitisha sheria ilioifanya nchi hiyo kuwa Jamhuri na kusitisha utawala wa malkia. Ilijunga upya miaka 33 baadaye mnamo 1994 baada ya kumalizika kwa ubaguzi wa rangi nchini. Mnamo 2008 Jumuiya ya madola ilikubali kuirudisha Pakistan mwaka mmoja baada ya kuusitishauwanachama wake kufuatia hatua ya kiongozi aliyekuwepo Pervez Musharaf kuidhinisha hali ya hatari na kuwazuia maelfu ya wanaharakati wa upinzani. Gambia ilijiunga na jumuiya ya madola kwa mara ya kwanza mnamo 1965, muda mfupi tu baada ya kupata uhuru kutoka kwa Uingereza. Ombi la Gabon mwaka jana kurudi katika jumuiya ya madola liliitikiwa na wengi, na sasa Gambia imerudi rasmi na imealikwa kuhudhuria mkutano wa viongozi wa serikali wa jumuiya ya madola huko London mwezi Aprili. Kwa sasa kuna mataifa 53 katika jumuiya hiyo. Kwa hisanio ya BBC.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.