Mapigano mapya yameibuka mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo katika jimbo la Kivu Kaskazini Mapema asubuhi ya leo Jumatano.
Vyanzo vya habari vinasema kuwa vikosi vya serikali vinapigana kuchukua tena vijiji katika eneo la Rutshuru, ambalo kwa sasa linadhibitiwa na waasi wa M23.
Mkazi wa mji wa mpakani wa Bunagana ameiambia BBC kwamba wamesikia milio ya silaha nzito kwa umbali.
M23 walitangaza usitishaji wa mapigano tarehe Aprili moja, ili kutoa fursa ya mazungumzo na serikali.
Viongozi wa kikanda walitarajiwa kukutana kwa ajili ya mazungumzo ya amani mwishoni mwa juma hili.