Mahakama ya kijeshi nchini Burkina Faso imemuhukumu rais wa zamani Blaise Compaore kifungo cha maisha gerezani kwa kuhusika katika mauaji ya mtangulizi wake Thomas Sankara mwaka 1987.
Compaore, ambaye yuko uhamishoni, amehukumiwa kifungo hicho bila kuwepo.
Mkuu wake wa usalama, Hyacinthe Kafando, pia amehukumiwa kifungo cha Maisha jela.
Bwana Sankara, mwanamapinduzi aliyekuwa na itikadi za Kimarxist, aliuawa kwa kupigwa risasi na kundi la watu wenye silaha katika mji mkuu, Ouagadougou mwaka 1987.
Baada ya mauji hayo Compaore alitawala kwa miaka 27 kabla ya kupinduliwa mwaka 2014.
#ChanzoBBC