Star Tv

Wafuasi wa mgombea wa upinzani wa Zambia Hakainde Hichilema wameanza kusherehekea wakati matokeo ya kwanza yaliyotolewa leo Jumamosi na tume ya uchaguzi yakionyesha kuwa kiongozi huyo wa upinzani anaongoza.

Matokeo ya kwanza yaliyotolewa na tume ya uchaguzi ya Zambia yanaonyesha kuwa kiongozi wa upinzani Hakainde Hichilema, amechukua uongozi wa mapema dhidi ya Rais aliyeko madarakani Edgar Lungu.

Tume ya uchaguzi ya Zambia imewahimiza watu kuwa watulivu wanaposubiri matokeo rasmi ya mwisho ili kuepuka machafuko.

Chini ya asilimia 20 ya kura zilizohesabiwa kati ya maeneo bunge 156, Hichilema anaongoza kwa kura 449,699 dhidi ya Rais Lungu mwenye kura 266,202.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Patrick Nshindano amesema matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo yanatarajiwa kutangazwa siku ya Jumatatu.

Wagombea 16 wa Urais waliwania wadhifa huo wakati wengine tayari wamekubali kushindwa na kumpongeza Hichilema kwa ushindi, wakinukuu matokeo yaliyotolewa hadi sasa katika vituo kadhaa vya kuhesabu kura.

#ChanzoDWSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.