Star Tv

Kiongozi wa zamani wa Baraza la jeshi nchini Mali Kanali Assimi Goïta amejitangaza kuwa rais wa mpito baada ya kuwavua madaraka rais wa mpito na Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo.

Rais Bah Ndaw na Waziri Mkuu Moctar Ouane waliokuwa katika kambi ya kijeshi usiku wa Jumatatu kwasasa wameachiwa huru kutoka kizuizi cha kijeshi.

viongozi hao walipelekwa katika kambi ya kijeshi usiku wa Jumatatu katika hatua ambaye iliifanya Mali kukabiliwa na mapinduzi ya pili ya kijeshi ndani ya miezi tisa.

Hatua hiyo ilichochewa na mageuzi katika baraza la mawaziri ambapo maafisa wawili wa jeshi waliohusika na mapinduzi ya awali walipoteza kazi zao.

Kanali Goïta alilalamika kwamba rais aliyeondolewa madarakani hakushauriana naye kuhusu baraza jipya la mawaziri.

Aidha, Hali ya taharuki imetanda nchini Mali hivi leo lakini mpaka sasa imeripotiwa kuna utulivu.

ChanzonaBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.