Star Tv

Wizara ya afya nchini Uganda imetangaza wagonjwa wanne wapya wa virusi vya corona na kufanya idadi ya walioathirika na ugonjwa huo kufikia 79.

Wagonjwa hao wanne ni madereva wa malori kutoka Tanzania waliowasili nchini humo kupitia mpaka wa Mutukula.

Wagonjwa hao ni miongoni mwa sampuli 1,578 zilizochukuliwa kutoka kwa madereva wa malori, ambapo miongoni ni kati ya sampuli za wakazi 411 zilizochukulia ili kufanyiwa vipimo hakuna hata mtu mmoja aliyekutwa na ugonjwa huo isipokuwa madereva hao.

Hatua hiyo inajiri siku chache baada ya Uganda kuwarudisha nyumbani kwa lazima raia wawili, huku mmoja akiwa ni wa Tanzania na mwingine wa Kenya ambao walikutwa na virusi hivyo.

Aidha, uamuzi huo ulidaiwa kuathiri uhusiano kati ya mataifa hayo wanachama wa Afrika mashariki na hivyo kuhatarisha usafirishaji wa mizigo kati ya nchi hizo.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.