Wizara ya Afya nchini Uganda imethibithisha kuwa watu wenye maambukizi ya Virusi vya Corona nchini humo wamefikia 74 baada ya watu 11 kupimwa na kubainika wameambukizwa virusi hivyo.
Kati ya wagonjwa hao 11 watu sita ni raia kutoka Tanzania ambao ni madereva wa magari ya mizigo, na watano wanatoka nchini Kenya.
Wizara ya Afya nchini humo imetoa taarifa ya wagonjwa 46 kupona na kuruhusiwa kurejea nyumbani huku hakuna kifo chochote kilichoripotiwa.
Aidha, visa hivi vinaendelea kuongeza huku katazo la Rais Museven alilowataka watu kuendelea kusalia ndani nyumbani bado likiwa halijaondolewa nchini humo.