Star Tv

Wizara ya Afya Uganda imetangaza ongezeko la mgonjwa mmoja wa COVID-19, ambapo mgonjwa huyo mmoja wa Corona aliyetangazwa leo anaongeza idadi ya walioambukizwa ugonjwa huo nchini humo kufikia 56.

Wizara hiyo imesema mgonjwa huyo mpya ni mkimbizi kutokea Burundi mwenye umri wa miaka 46 ambaye aliingia Uganda alitokea Tanzania na tayari amewekwa Karantini anapata uangalizi pamoja na matibabu.

Mpaka kufikia aprili 14, watu 54 waligunduliwa kuwa na maambukizi ya virusi hivyo na kati yao wanne walitolewa taarifa yakuwa wamepona.

Marufuku yakukaa ndani ilitangazwa Machi 31 na rais Museveni ambapo aliwataka watu kutokutoka nje kwa siku 14 ambazo ziliisha Aprili 14.

Aprili 14, 2020 wakati akizungumza na vyombo vya habari Museveni aliongeza muda wa siku 21 kwa ajili ya watu kuendelea kusalia majumbani ili kupambana na virusi vya ugonjwa huo, Hatua hiyo inachukuliwa kama njia ya kupunguza kuenea kwa maambukizi ya Virusi vya Corona.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.