Star Tv

Waziri wa Usafirishaji wa Kenya James Macharia amesema wanatarajia kutuma ndege ya Kenya Airways nchini China siku ya Jumatano kwa ajili ya kuchukua vifaa vya kupambana na ambavyo vitatumika kuzuia kuenea kwa maambukizi ya Corona ugonjwa.

Waziri Macharia ametoa taarifa hiyo wakati akitangaza kuongezwa muda wa marufuku ya ndege za kigeni kuingia nchini Kenya kwa muda wa siku 30 nyingine, na kuruhusu ndege za mizigo tu na zile za kuhamisha raia wa kigeni ambazo zitaendelea kufanya kazi.


Aidha, nchi ya Kenya imethibitisha kuwa na wagonjwa wapya 16 wa corona, baada ya kuwafanyia vipimo watu 530, na mpaka sasa Kenya imefikisha idadi ya watu 142 wenye maambukizi ya COVID-19.

Wizara ya Afya ya Kenya imetangaza kuwa katika kesi hizo mpya 16 za maambukizi ya corona nchini humo, raia wa Kenya ni 15 na mmoja ni raia wa Nigeria, raia 11 kati ya hao wana historia ya kusafiri nje ya nchi na watano kati yao wameambukizwa wakiwa ndani ya Kenya, watu 12 ni kutoka mji mkuu wa Kenya Nairobi, wengine watatu wanaishi Mombasa na mmoja ni kutoka Kilifi.

Waliokutwa na maambukizi mapya wana umri kati ya miaka 22 na 66, wanaume ni tisa na wanawake saba.


Vilevile Wizara ya Afya ya Kenya imesema kuwa inatengeneza barakoa (maski) ambazo zitasambazwa kwa wananchi hivi karibuni, na pia imesema watu watakaokufa kwa corona watazikwa ndani ya masaa 24 huku watu wa karibu wa familia wasiozidi 15 ndio wataruhusiwa kuhudhuria mazishi hayo yatakayosimamiwa na Serikali.

                        Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.