Star Tv

Maafisa wa polisi mjini Nakuru, Kenya wanamzuilia mwanamume anayedaiwa kuwauzia watu nyama ya paka.

Mwanamume huyo alikamatwa Jumapili ambapo inadaiwa alipatikana akimchuna ngozi paka. James Mukangi Kimani anadaiwa kuwauzia wauzaji wa samosa nyama hiyo, na pia kuuzia wenye migahawa.

Gazeti la Star linasema mwenyewe alikiri kupika samosa akitumia nyama hiyo.

Taarifa kwenye vyombo vya habari Kenya zinasema mwanamume huyo alikiri kuuza nyama ya paka zaidi ya elfu moja mjini humo tangu mwaka 2012.

Gazeti la Nation linasema aliwaambia wanahabari kwamba alianza 'biashara' hiyo baada ya "kugundua kulikuwa na pengo sokoni".

Alisema huwa anauza pia ngozi za paka na kwamba kwa kila paka hujipatia takriban Sh500 (Dola 5 za Marekani).

"Huwa nawaambia wateja wangu kwamba huwa naipata nyama hii kutoka Gioto (jaa la kutupa taka), lakini huwa hawajui kwamba ni nyama ya paka," alinukuliwa na gazeti la Nation.

Mwanamume huyo alifumaniwa eneo la Railways, Nakuru na alipigwa na umati wa watu kabla ya kuokolewa na maafisa wa polisi na kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Ukulima.

Chini ya sheria za Kenya, ni haramu kula nyama ambayo haijakaguliwa na afisa wa afya ya umma, na pia kula nyama kutoka kwa mnyama ambaye haruhusiwi kuliwa Kenya.

Paka si miongoni mwa wanyama wanaoruhusiwa kuliwa chini ya Sheria za Kudhibiti Nyama Kenya. Mwanamume huyo anatarajiwa kufikishwa kortini leo Jumatatu.

Kwa hisani ya BBC

Picha na mtandao.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.