Star Tv

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM umempitisha Dkt Hussein Mwinyi kuwa mgombea wa Urais wa Zanzibar baada ya kupata kura 129 sawa na asilimia 78.65 akiwashinda wenzake wawili Shamsi Vuai Nahodha na Dkt. Khalid Salim Mohamed.

Awali Katibu Mkuu wa Chama cha CCM Dkt.Bashiru Ally alitaja majina matatu kutoka majina matano yaliyokuwa yamepitishwa na Kamati Kuu Maalum kuwania nafasi ya urais Zanzibar. Majina hayo matatu yaliyokuwa yametajwa kupita ni Dkt. Hussein Mwinyi, Shamsi Vuai Nahodha pamoja na Dkt. Khalid Salum Mohammed.

Dkt. Hussein Mwinyi ni miongoni mwa majina matatu yaliyotajwa leo Julai 10,2020 kwenye ufunguzi wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika katika ukumbi wa White House Dodoma na kupigiwa kura ndani ya ukumbi huo kutoka kwa viongozi mbalimbali ndipo Dkt.Hussein Mwinyi akatajwa kuibuka kidedea ambaye anatarajiwa kushindana na mgombea kutoka chama cha upinzani kuwania kiti cha Urais Zanzibar

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.