Star Tv

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam linawashikilia watu 32 watuhumiwa wa wizi wa shilingi Bilioni 2.82 za benki ya NMB wakiwemo wafanyakazi watano wa kampuni ya ulinzi iliyopewa jukumu la kulinda wakati fedha hizo zikihamishwa kutoka tawi la benki hiyo la Mbezi Beach kwenda NMB House Posta Mpya na kutokomea kusikojulikana na gari iliyobeba fedha hizo.

Hata hivyo Jeshi hilo limekamata gari hiyo na kukuta masanduku matatu yenye shilingi Bil. 1.3 na silaha aina ya short gun pump Action yenye risasi 12 na short gun protector yenye risasi 5 na sare za kampuni hiyo ya ulinzi.

Jeshi hilo limesema limefanya juhudi za kuhakikisha fedha hizo ambazo ni mali za Watanzania zinapatikana, na kusema kuwa watu hao walioshiriki katika wizi wa fedha hizo japokuwa tayari walishanunulia vitu vya thamani kwa njia ya utakatishaji fedha na tayari wameshawakamata.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.