Star Tv

Wananchi wa Malawi wanapiga kura leo katika marudio ya Uchaguzi wa urais, katika Uchaguzi ambao unaelezwa na wachambuzi kama kipimo cha demokrasia katika taifa hilo.

Hatua hii imekuja baada ya Mahakama kufutilia mbali ushindi wa rais Peter Mutharika mwezi Februari baada ya kubainika kwa udanganyifu na kuagiza uchaguzi mpya.

Rais Mutharika anatarajiwa kupata ushindani mkali kutoka kwa kiongozi wa upinzani Lazarus Chakwera, huku kila mmoja akisema ana uhakika wa kushinda.

Mahakama mwezi Februari ilisema ushindi wa rais Peter Mutharika uligubikwa na udanganyifu mkubwa.

Mahakama ya Katiba ilichukuwa uamuzi wa kufutilia mbali uchaguzi huo kutokana na dosari nyingi zilizoufanya uchaguzi huo usiwe huru, haki na wa kuaminika, alisema Jaji kiongozi wa Mahakama ya Katiba, Healey Potani.

Katika uchaguzi huo uliofanyika Mei 21 mwaka 2019, Tume ya uchaguzi ilimtangaza Peter Mutharika kuwa mshindi wa uchaguzi kwa kupata asilimia 38.6 ya kura zote.

Uchaguzi unafanyika chini ya sheria mpya, ambapo mshindi sasa atahitaji kupata wingi wa kura wa 51% .

Kwa miezi kadhaa sasa, raia wa Malawi wamekuwa katika mgogoro wa kisiasa ambao haujawahi kushuhudiwa katika historia ya nchi hiyo. Ni zaidi ya mwaka sasa tangu mamilioni ya raia walipojitokeza katika uchaguzi wa bunge na urais.

Kumekuwa na maandamano ya kupinga serikali pamoja na kutokea kwa ghasia ambako kumetishia nchi hiyo kutumbukia katika mgogoro mkubwa zaidi.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.