Star Tv

Ikiwa leo ni Siku ya Wauguzi Duniani, Wauguzi nchini wametoa rai kwa wauguzi wote walioko katika hospitali mbalimbali kuwa na kauli nzuri, upendo kwa wagonjwa wanaowahudumia kwakuwa kauli ya muuguzi inaweza kumfariji mgonjwa pamoja na kuthamini utu wa wagonjwa.

Kwa upande wake Bilha Melita ambaye ni mwekahazina wa Chama cha Wauguzi Arusha ameiomba jamii kuacha kuwa na mtazamo mbaya kwa wauguzi kwakuwa wengi wao wamejirekebisha na kwasasa na hawatoi kauli mbaya kwa wagonjwa kama inavyosemekana isipokuwa kila mtu ana tabia zake.

Muuguzi aitwaye Sofia Sanga kutoka Dar es Salaam amefafanua kuwa kwa zama zimebadilika sio kama zamani na Muuguzi ni msaidizi wa wagonjwa na sio msaidizi wa daktari kama wengi wanavyodhani.

Makamu wa rais wa Chama cha Wauguzi Tanzania Ibrahimu Mgoo amesema Wauguzi wanajitahidi kufanya vyema kazi zao japo kuwa muda mwingine wanakumbana na hali ngumu ikiwemo uchache wao hususani katika kipindi hiki cha Ugonjwa huu wa COVID-19 na kuiomba serikali iliangalie suala hili.

Yote haya wameyazungumza kupitia kipindi cha Tuongee Asubuhi kinachorushwa na StarTv ambapo wote hao wamewataka wauguzi wote nchini kuitumia vyema taaluma yao namna inavyowapasa.

Aidha, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la afya WHO katika maadhimisho ya siku hii, umesema mchango wa wahudumu hawa wa afya hauna kipimo hasa wakati huu ambao janga la virusi vya corona linaitikisa dunia.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.