Star Tv

Shirika la Afya Duniani limesihi watu kutoweka imani zao kwa dawa za mitishamba zinazotengenezwa na wenyeji kwa misingi ya kudai zina uwezo wa  kukabiliana na virusi vya corona.

Hatua hiyo imekuja baada ya marais karibu wanne wa Afrika kusema wanaagiza dawa ya mitishamba iliyosemekana imepatikana Madagascar kuwa ina uwezo wa kutibu virusi vya corona.

Shirika la Afya Duniani limepata taarifa zao na kutoa onyo juu ya dawa hizo wakati ambapo kila mmoja duniani ana hamu ya kupata dawa ya kutibu ugonjwa huo.

Shirika hilo limesema ni muhimu dawa zinazosemekana kuwa na uwezo wa kutibu kufanyiwa majaribio kabla hazijaanza kutumika na kuonya kuwa huenda watu wakaona wamepata tiba na kujihisi kuwa salama na kumbe hazina uwezo wa kutibu.

Viongozi wa Afrika ambao tayari wamezungumzia kwenda kuchukua dawa hiyo ni rais Magufuli, rais wa Jamuhuri ya Congo, Guinea Bissau na Equatorial Guinea.

Dawa hiyo inayohusishwa na mmea wa Kichina unaoitwa Artemisia(pakanga) ambao ni mojawapo ya miti ambayo huchanganywa pamoja na mimea mingine ya Madagascar kama tiba ya ugonjwa wa Malaria.

Aidha, rais wa Madagascar Andry Rajoelina amesema nchi yake itaanza majaribio ya kitabibu ya kinywaji cha mitishamba ambacho anakipigia upatu kuwa kinauwezo wa kuzuia na kutibu corona.

Pia amewataka wananchi wake kupanda kwa wingi mmea ambao unaotomika kutengeneza kinywaji hicho ambacho kimepewa jina la Covid-Organics.

Rais Rajoelina amesema kwa sasa anatafuta kibali cha WHO ili kuwa kinywaji hicho kuwa dawa ya kutibu Corona.

Hata hivyo msimamo wa Shirika la Afya kuhusu kinywaji hicho mpaka sasa haujabadilika na wanaonya watu dhidi ya dawa mbadala kutumika kama kinga ama tiba ya corona.

Mpaka kufikia sasa watu zaidi ya milioni 3.5 duniani kote wamethibitishwa kupata maambukizi ya virusi vya corona, watu zaidi ya laki mbili na hamsini wamefariki dunia huku watu zaidi ya milioni moja wamepona.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.