Star Tv

Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa amelitaka shirika la viwango nchini TBS na tume ya ushindani FCC kuacha kukaa ofisini badala yake wachunguze bei na uzalishwaji wa bidhaa za kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona ili ziweze kupatikana kwa urahisi na kwa bei elekezi.

Tamko hili limekuja siku chache mara baada ya serikali kupitia wizara ya afya kuthibitisha uwepo wa virusi vya corona nchini, upatikanaji wa bidhaa za usafi wa mikono yaani sanitizer, barakoa na vitakasa mikono pamoja na kemikali za usafi wa mazingira katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam umekuwa na changamoto kutokana na kupanda kwa bei,

Mbali na changamoto hiyo lakini bado kiwango halisi kinachohitajika katika vitakasa mikono hivyo kimekua na sintofaghamu pamoja na bei elekezi inayopaswa kufuatwa na wauzaji wa bidhaa hizo.

Waziri Bashungwa baada ya kusikia hayo akatumia nafasi hiyo kutembelea baadhi ya viwanda vinavyofanya uzalishaji wa bidhaa za vitakasa mikono kuangalia namna ambayo serikali inaweza kuwaongezea uwezo ili kuzalisha bidhaa hizo kwa wingi na kukidhi mahitaji yaliyopo sasa.

Mbali na kutembelea viwanda hivyo, imedhihirika kuwa viwanda vilivyopo sasa nchini  vina uwezo wa kuzalisha vitakasa mikono lita 5000 kwa siku huku huitaji ukiwa ni lita laki tatu na elfu hamsini.

Serikali imesema haitasita kuwachukulia hatua za kisheria ikiwemo kuwanyang’anya leseni wafanyabiashara ambao watabainika wanatumia mlipuko wa virusi vya corona kama sehemu ya kujipatia faida kubwa.

                                                                  Mwisho.

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.