Star Tv

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa ameonya utoaji taarifa za holela na upotoshwaji kuhusu ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababisha na virusi vya corona (COVID 19) unaofanywa na watu mbalimbali nchini.

Waziri Mkuu ametoa onyo hilo wakati akizungumza na Wakuu wa Mikoa yote nchini, Makatibu Tawala wa Mikoa na Waganga Wakuu wa Mikoa kwa njia ya video kutokea ofisini kwake Mlimwa jijini Dodoma.

Amezungumzia wajibu wa viongozi husika kuwa ni kushirikiana na mganga mkuu wa mkoa na wale wote walioko katika sekta ya tiba kuimarisha uratibu wa ugonjwa huu ndani ya mkoa.

Waziri Mkuu ameiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA ifuatilie watu wote wanaofanya upotoshaji kupitia mitandao ya kijamii ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Amewataka wakuu wa mikoa waimarishe utoaji wa elimu kwa umma ili wananchi waelewe athari za ugonjwa huo na namna ya kujikinga pamoja na kuwaondolea hofu waweze kuendelea na shughuli zao za kimaendeleo.

                             Mwisho

 

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.