Star Tv

Waziri  wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo  ametoa maagizo kwa wakuu wa wilaya,wakurugenzi na wakuu wa shule nchini,kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri wa usafiri kwa wanafunzi wote ambao wamekosa usafiri wa kurudi nyumbani mara baada ya shule zote kufungwa kufuatia uwepo wa ugonjwa Corona nchini.

Hii ni mara baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutoa tamko mnamo Machi 17,2020, la kufunga shule zote za awali, msingi na sekondari, vyuo vya kati pamoja na vyuo vikuu kwa siku 30 kutokana na tishio la ugonjwa wa Corona.

Waziri Jafo ametoa kauli hiyo leo Machi 20,2020 ofisini kwake jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa iwapo kuna shida inayowafanya wakuu wa shule washindwe kuweka utaratibu mzuri wa wanafunzi wote kurejea nyumbani   wawasiliane na wenyeviti wa kamati za ulinzi na usalama ambao ni wakuu wa wilaya.

Aidha Mhe.Jafo ametoa  pongezi kwa Mkuu wa Shule ya Kilakala iliyopo Morogoro na Mkuu wa Shule ya Dodoma Sekondari kwa kuweka utaratibu mzuri uliowezesha wanafunzi wote kurudi nyumbani hata kwa ambao wazazi wao hawakuwa na hela za nauli wameweza kufika bila ya shida yoyote.

                  Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.