Tume ya Afya na Magonjwa ya China imesema kuwa wagonjwa wapya 889 wamethibitika kuambukizwa virusi vya Corona hadi kufikia siku ya jana.
Taarifa iliyotolewa leo imeeleza kuwa idadi hiyo imeongezeka kutoka 394 iliyoripotiwa siku moja kabla.Jumla ya idadi ya watu walioambukizwa virusi vya Corona China bara hadi sasa imefikia 75,465.
Aidha, idadi ya watu waliokufa kutokana na virusi hivyo ni 2,236, Huku jimbo la Hubei ambako ndipo virusi hivyo vilianzia imetangaza vifo vipya 115 na kwenye mji wa Wuhan watu 99 wamepoteza Maisha kutona na virusi hivyo.
Wakati huo huo, Korea Kusini imethibitisha visa vipya 52 vya virusi vya Corona na hivyo kuifanya idadi ya watu walioambukizwa virusi hivyo kufika 156.
Idara ya kudhibiti magonjwa ya Korea Kusini, imesema visa vipya 39 vimethibitishwa katika mji wa kusini wa Daegu.
Mwisho.