Star Tv

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira ameuagiza uongozi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA kuchukua hatua za dharura ili kuimarisha hali ya usalama  uwanjani hapo kwa kuongeza mitambo ya kubaini watu wenye vimelea vya

Taarifa na Zephania Renatus

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira ametoa kauli hiyo alipotembelea Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA  akiongozana na kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa  kwa lengo la kuangalia hatua zinazochukuliwa uwanjani  hapo katika kukabili Magonjwa ya mlipuko .

Kauli hiyo imefuatiwa na taarifa zilizodokeza  kuwa ,uwanja huo una mtambo mmoja tu wa kubaini endapo mgeni yoyote ataingia nchini akiwa na dalili za magonjwa  ya mlipuko  ikiwemo  virusi vya corona vinavyotajwa kuendelea kuua mamia ya raia wa china..

Pamoja na hayo,Mkurugenzi mtendaji katika Uwanja wa KIA Mhandisi Christopher Mukoma amesema idara ya kitengo cha afya  bado inakabiliwa na upungufu wa watumishi.

Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA  umekuwa ni lango la kuingia na kutoka ,na zaidi ya wageni elfu mbili kutoka mataifa mbalimbali wamekuwa wakiingia na kutoka kwa kila siku kupitia lango hilo.

                                                                             Mwisho

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.