Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira ameuagiza uongozi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA kuchukua hatua za dharura ili kuimarisha hali ya usalama uwanjani hapo kwa kuongeza mitambo ya kubaini watu wenye vimelea vya
Taarifa na Zephania Renatus
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira ametoa kauli hiyo alipotembelea Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA akiongozana na kamati ya ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa lengo la kuangalia hatua zinazochukuliwa uwanjani hapo katika kukabili Magonjwa ya mlipuko .
Kauli hiyo imefuatiwa na taarifa zilizodokeza kuwa ,uwanja huo una mtambo mmoja tu wa kubaini endapo mgeni yoyote ataingia nchini akiwa na dalili za magonjwa ya mlipuko ikiwemo virusi vya corona vinavyotajwa kuendelea kuua mamia ya raia wa china..
Pamoja na hayo,Mkurugenzi mtendaji katika Uwanja wa KIA Mhandisi Christopher Mukoma amesema idara ya kitengo cha afya bado inakabiliwa na upungufu wa watumishi.
Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro KIA umekuwa ni lango la kuingia na kutoka ,na zaidi ya wageni elfu mbili kutoka mataifa mbalimbali wamekuwa wakiingia na kutoka kwa kila siku kupitia lango hilo.
Mwisho