Star Tv

Waziri mkuu wa Urusi Dmitry Medvedev amewasilisha barua yake ya kujiuzulu kwa rais Vladmir Putin leo.

Rais Putin alikutana na waziri Medvedev baada ya rais  huyo kutoa hotuba yake kupitia televisheni ya taifa ambapo amependekeza kufanyia mageuzi katiba ili kulipa bunge uwezo wa kumteua waziri mkuu kwani katiba iliyopo kwasasa inampa  rais mamlaka ya kumteua waziri mkuu.

Taarifa zinaeleza kuwa Medvedev alinukuliwa akisema kuwa katika muktadha huu ni wazi kwamba , baraza la mawaziri , linapaswa kumpatia rais wa nchi fursa hiyo ya kuchukua hatua zote zinazostahili.

Aidha, Rais Putin alinukuliwa akimuelekeza Medvedev kuendelea kuwa katika wadhifa wa waziri mkuu hadi pale baraza jipya la mawaziri litakapoundwa.

Katika hotuba yake kwa taifa Rais Putin alisema kuwa Medvedev atateuliwa kuwa naibu mkuu wa baraza la taifa la usalama nchini humo ambapo  Putin ni mkuu wa baraza hilo.

                                                                                     Mwisho.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.