Star Tv

 Watoto 26 wamekufa katika ajali ya moto uliounguza shule moja ya Kiislamu karibu na mji mkuu wa Liberia, Monrovia.

Ofisi ya rais wa nchi hiyo imesema hayo leo na kuongeza kwamba maafisa wa kutoa huduma za dharura wamemwambia Rais George Weah kwamba jumla ya watu 28, wamekufa kufuatia mkasa huo ambao umetokea usiku wa kuamkia leo. Afisa mmoja wa jamii ya Fulani Amadou Sherrif amesema moto ulitokea wakati watoto walikuwa wakilala. Msemaji wa ikulu Solo Kelgbeh amesema Rais Weah tayari amezuru eneo la Paynesville ilikotokea ajali hiyo ya moto. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Weah ametuma rambirambi zake kwa familia ambazo zimewapoteza wapendwa wao. Ndugu na jamaa wamekusanyika nje ya lango kuu la jengo ambalo ndani yake kulikuwa na shule hiyo ya bweni ambayo paa lake limeteketea.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.