Star Tv

Maafisa wa usalama nchini Afrika Kusini hapo jana walikabiliana na waporaji kwa kutumia magurunedi na risasi za mpira katika juhudi za kutawanya makundi yaliokuwa yakilenga biashara zinazomilikiwa na raia wa kigeni nchini humo katika eneo la katikati mwa mji wa Johannesburg.

Mtu mmoja aliuawa na wengine watano kujeruhiwa. Ghasia hizo ni za punde zaidi za mashambulizi dhidi ya raia wa kigeni mjini humo na maeneo mengine nchini humo. Takriban watu 10 wameuawa katika mashambulizi hayo ambayo pia yamechochea maandamano katika mataifa mengine barani Afrika. Baadaye kupitia ujumbe katika mtandao wa twitter, polisi wamesema kuwa hali hiyo imedhibitiwa. Msemaji wa polisi Xlolani Fihla amethibitisha kifo hicho kwa shirika la habari la AFP kufuatia ghasia hizo za jana ijapokuwa hakuweza kuthibitisha chanzo cha kifo hicho.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.