Na katika michezo , mashindano ya fainali za kombe la mataifa ya Afrika AFCON yanayoendelea nchini Misri, jana Cote d'Ivoire iliishinda Afrika kusini kwa bao 1-0, nayo, Tunisia ikatoka sare ya bao 1-1 na Angola na Mali iliirarua Mauritania kwa mabao 4-1.
Leo kundi F linaingia dimbani wakati mabingwa watetezi cameroon itakapotiana kifuani na Gzinea Bissau na Ghana ina miadi na Benin. Wakati huo huo mlinzi wa Senegal Salif Keita ambaye anachezea klabu ya Ujerumani ya Schalke o4 atakosa michezo karibu miwili ya mashindano hayo baada ya kupata maumivu katika kifundo cha mguu katika ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania siku ya Jumapili, limesema shirikisho la kandanda la Senegal jana.
CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW