Star Tv

Tanzania imeendelea kuweka juhudi za kuimarisha miundombinu ya usafirishaji ikiwemo kuimarisha bandari ya Dar es Salaam na Mtwara, kujenga bandari kavu na kukamilisha ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mbambabay ambayo itawawezesha wafanyabiashara wa Malawi kutumia bandari ya Mtwara.

Hayo yamejiri katika ziara ya TPA pamoja na wadau mbalimbali kama TATOA, TRA, TAZARA, TAFFA, TICTS, DCG, katika kukagua miundombinu ya usafirishaji wa mizigo ya wafanyabiashara wa Malawi kuitikia maelekezo yaliyotolewa na Rais, DK; John Magufuli wakati wa ziara yake Aprili 24, mwaka huu nchini Malawi. Rais DK; Magufuli aliagiza TPA pamoja na wadau wa sekta ya usafirashaji na wadau wengine kutatua kero zinazowakabili wafanyabiashara wa Malawi ili waweze kutumia bandari ya Dar es Salaam. Aidha kujengwa kwa bandari kavu na kukamilishwa kwa ujenzi wa barabara ya Mtwara-Mbambabay kutawezesha wafanyabiashara wa Malawi kutumia bandari ya Mtwara ambayo iko umbali mfupi wa kilometa 820.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.