Star Tv

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed amewasili mjini Kharotum, Sudan kusimamia mazungumzo kati ya baraza la kijeshi na viongozi wa waandamanaji kufuatia hatua kali za kijeshi dhidi ya waandamanaji wiki hii.

Kulingana na shirika la habari la AFP Abiy ataongoza mikutano kati yake na watawala wa kijeshi na baadaye atakutana kwa mazungumzo na viongozi wa waandamanaji lakini kwa nyakati tofauti. Ziara yake inakuja baada ya Umoja wa Afrika wenye makao yake Addis Ababa Ethiopia, kusimamisha uanachama wa Sudan kufuatia mzozo wa kisiasa nchini humo. Kulingana na jumuiya ya madaktari nchini Sudan, watu 113 wameuawa kufuatia hatua hizo kali za kijeshi zilizoanza kuchukuliwa siku ya Jumatatu kwa lengo la kuwatawanya waandamanaji.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.