Star Tv

Watu sita wamefariki dunia na wengine kadhaa hawajulikani walipo, kufuatia mvua kubwa zilizosababisha maporomoko ya udongo katika wilaya ya Bududa mashariki mwa Uganda.

Shirika la Msalaba mwekundu la Uganda limesema karibu watu 50 wanaaminika kutojulikana walipo na nyumba 150 zimeharibiwa usiku wa Jumanne katika eneo la chini ya mlima Elgon. Shirika hilo limesema miongoni mwa waliokufa ni bibi wa miaka 73 na watoto watatu, na kuongeza kuwa watu wasiopungua 27 walijeruhiwa na karibu 350 wamelaazimika kuyapa kisogo makaazi yao. Limesema vifo zaidi vinatarajiwa mnamo wakati mvua zikiendelea kunyesha na uwezekano wa kuzuka kwa ugonjwa wa nemonia miongoni mwa watoto, na miripuko ya kipindupindu na kuharisha. Wilaya ya Bududa ilioko kwenye mpaka kati ya Uganda na Kenya, ni eneo la hatari kubwa ya kukumbwa na maporomoko ya udongo.

CHANZO: Idhaa ya Kiswahili DW

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.