Star Tv

Uongozi wa Hospital ya rufaa ya mkoa wa Mara umelazimika kufunga kamera maalumu katika maeneo yote ya hospitali hiyo ili kukabiliana na matatizo ya wizi wa vifaa tiba na vitisho toka kwa ndugu wa wagonjwa kuwapiga wauguzi pindi wanapotoa huduma.

 Mganga mfawidhi wa hospital ya rufaa ya mkoa wa Mara Dr Joakim Eyembe amefanya mazungumzo  na wauguzi baada ya kusikiliza kero zinazowakabili juu ya vitisho toka kwa ndugu wa wagonjwa na wizi wa vifaa tiba  amewaondoa hofu kwa kuwaambia tayari kamera zimefungwa kila sehemu. Dr Eyembe ameongeza kuwa wameamua kuajiri kampuni maalumu ya ulinzi ili kuweza kukabiliana na tatizo la wizi wa vifaa tiba ufanywao na vijana wanaoingia kwa kupitia katika uzio. Hayo yamejiri katika kilele cha siku ya wauguzi duniani kilichofanyika katika viwanja vya hospital hiyo huku wauguzi wakitoa huduma mbali mbali kwa wagonjwa.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.