Star Tv

Wafungwa wanne kati ya sita wa Kipalestina waliotoroka kutoka jela yenye ulinzi mkali mapema wiki hii wamekamatwa, polisi wa Israeli wanasema.

Wawili walipatikana katika maegesho ya magari mapema asubuhi ya Jumamosi, polisi walisema.

Msako ulianzishwa Jumatatu baada ya wafungwa hao sita kutoka nje ya gereza la Gilboa Kaskazini mwa Israel, Ambapo ni tukio la kwanza la kutoroka gereza la Palestina kwa miaka 20.

Makundi ya wapiganaji wa Palestina wakati huohuo yalisifu kutoroka kwao wakikiita kitendo hicho kuwa cha "kishujaa".

Wafungwa hao waliotoroka wanaaminika kuchimba shimo kwenye sakafu ya gereza lao kwa miezi kadhaa na kuweka shimo kuelekea chini ya gereza.

Wanafikiriwa kutambaa kupitia shimo hilo na kufikia ukuta wa nje wa gereza, kisha wakachimba handaki lililoibuka katikati ya barabara ya udongo, chini tu ya mnara wa walinda usalama.

Picha za CCTV ziliwanasa wakiacha handaki saa 01:30 Jumatatu. Lakini kengele ilipigwa saa 04:00 alfajiri baada ya wenyeji kuripoti kuona watu wanaoshukiwa kuwa wafungwa katika uwanja karibu na gereza.

Vyombo vya habari vya Israeli vimeshutumu kutoroka jela kwa wafungwa hao vikiashiria kuzorota kwa usalama.

Kulikuwa pia na ripoti ambazo hazijathibitishwa kuwa mlinzi huyo alikuwa amesimama kwenye mnara karibu na njia ya handaki alikuwa amelala wakati walipokuwa wakitoroka.

Mmoja wa waliokamatwa ni Zakaria Zubeidi, ni kamanda wa zamani wa Brigedi ya Al-Aqsa huko Jenin. Alikamatwa na vikosi vya Israel mnamo 2019 kwa tuhuma za kuhusika katika mashambulio kadhaa ya risasi.

Wengine watano - Mahmoud Ardah, Mohammed Ardah, Iham Kamamji, Yaqoub Qadri na Munadil Infaat - ni wafuasi wa kundi la wapiganaji la Islamic Jihad. Wanne kati yao wanatumikia vifungo vya maisha baada ya kutiwa hatiani kwa kupanga au kutekeleza mashambulio yaliyowaua Waisraeli.

#ChanzoBBCSwahili

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.