Rais wa zamani wa Mali Moussa Traoré amefariki dunia leo Jumanne Septemba 15,2020.
Chanzo kutoka familia yake kimeiambia Shirika la Habari la RFI Rais huyo wa zamani wa Mali amefariki ingawa hawakubainisha ugonjwa uliopeleka afariki.
Moussa Traoré, ambaye alizaliwa Septemba 25, 1936, alichukua hatamu ya uongozi wa nchi mwaka 1968 kabla ya kupinduliwa mwezi Machi 1991.
Rais Traoré alihukumiwa kifo, lakini mwaka 2020 Rais wa zamani Alpha Oumar Konaré alimsamehe.
Katika miaka ya hivi karibuni, Marehemu Traore amekuwa akisikilizwa sana miongoni mwa wanasiasa nchini Mali.