Star Tv

Mkufunzi wa zamani wa Everton na Manchester United david Moyes amechukua mahala pake Slaven Bilic, ambaye alifutwa kazi siku ya Jumatatu wakati klabu hiyo ikiwa katika nafasi ya kushushwa daraja.

Moyes amekuwa bila kazi tangu mwezi Mei wakati alipojiuzulu kama mkufunzi wa Sunderland baada ya klabu hiyo kushushwa daraja.

Mwenyekiti mwenza wa West Ham David Sullivan alisema kuwa mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 54 raia wa Uskochi ndio mtu anyefaa kurithi nafasi hiyo.

Aliongezea: Tunahitaji mtu mwenye uzoefu ,utambuzi wa ligi ya Uingereza na wachezaji wake na tunaamini kwamba David anaweza kuwaimarisha wachezaji.

Ni mtu anayeheshimika katika soka na ataleta motisha na mawazo mapya.

Alithibitisha na Everton kwamba ana uwezo na tunadhani kwamba West Ham ni klabu ambayo itampatia fursa David Moyes kuonyesha uwezo wake.

Mechi ya kwanza ya Moyes itakuwa dhidi ya Watford katika ligi ya Uingereza mnamo mwezi Novemba 19.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.