Bingwa namba 22 Duniani katika ubora wa Tennis Jack Sock amaefanikiwa kutwaa taji lake la kwanza la Paris master kwa kumfunga Filip Rajinovic kwa 5-7 6-4 6-1.
Kwa ushindi wa Sock sasa anapata nafasi ya kucheza fainal ya ATP tour dhidi ya Pablo carreno Busta raia wa Hispania huku akisubiri ushindani wa mabingwa wengine watakao shiriki katika fainal hizo.
Sock anaeonyesha ushindani mkubwa katika tennis huenda akaingia katika nafasi 10 za juu za viwango vya Tennisi Duniani vitavyotangazwa kabla ya Droo ya ATP Tour mjini London November 12-19.
Sock amekuwa mwamerika wa kwanza kushinda taji hilo la Paris Master tangu mwaka 1999 aliposhinda Andre Agassi.
Picha na mtandao