Star Tv

Mwanasoka Didier Drogba, mwenye asilia ya Ivory Coast, amefungua shule ya kwanza ya msingi. Shule hiyo inatarajiwa kuwasaidia maelfu ya watoto walioko vijijini kwenye mashamba ya kakao ya jamii ya Pokou-Kouamekro kupata elimu bora imearifiwa.

Katika sherehe za ufunguzi wa shule hiyo, Drogba alisema, tumeshughulika na mradi huu kwa miaka miwili na ninayo fahari kuona umekamilika.

Imani ya shirika langu daima imekuwa mara zote watoto wakipata fursa ya kupata elimu bora na huduma za afya zilizo bora, tutajenga kizazi chenye madaktari, wanasayansi, wafanya biashara wa kiume na wa kike na ndivyo tutakavyo ijenga Afrika iliyo bora zaidi.

Shule hiyo imejengwa chini ya ufadhili wa shirika la Didier Drogba, kwa ushirikiano mkubwa na kampuni ya Nestlé na mpango wa kimataifa wa uimarishaji zao la kakao .

Shule hiyo ina idadi ya vyumba vya madarasa sita, darasa la awali, kantini , maliwato, uwanja wa soka na nyumba za waalimu watatu.

Kwa hisani ya BBC.

Latest News

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Urusi Kuchagiza Maendeleo Afrika kupitia Nishati ya Nuklia na Madini ya Urani
12 Aug 2023 10:07 - Kisali Shombe

ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.