Watu sita wamefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari aina ya Toyota Noah iliyogongana na lori aina ya scania katika eneo la ALKATANI kata ya Sepeko tarafa ya Kisongo wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha katika barabara ya Arusha Babati.
Add a commentWaziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka taasisi za fedha kubuni mikakati na mbinu zitakazowezesha watanzania wengi zaidi kupata huduma rasmi za kibenki kwa gharama nafuu ili waweze kujiongezea kipato na kujikwamua na umasikini.
Add a commentRead more: TAASISI ZA KIFEDHA ZIBUNI HUDUMA NAFUU KWA WATANZANIA –MAJALIWA.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewaagiza wahandisi wa TARURA wasimamie miradi kwa weledi, uadilifu na uaminifu huku wakizingatia mikataba husika na pia wawe wabunifu kutumia teknolojia mpya, sahihi na rafiki kulingana na upatikanaji wa malighafi za ujenzi.
Add a commentRead more: “TARURA SIMAMIENI MIRADI KWA WELEDI NA UAMINIFU”-Mjaliwa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametangaza uamuzi wa Serikali wa kuondoa tozo 42 kati ya 47 ambazo walikuwa wanatozwa wakulima wa kahawa wa Mkoa wa Kagera hadi kufikia tozo 5 tu ambazo itakuwa ni jumla ya Shilingi 267 kwa kila kilo ya kahawa, kutoka Shilingi 830 za awali.
Add a commentRead more: TOZO 42 KATI YA 47 ZAFUTWA KWA WAKULIMA WA KAHAWA.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Innocent Bashungwa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani kwa kuwezesha ujenzi wa madarasa 15,000 ili wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza waweze kusoma bila msongamano.
Add a commentRead more: “TUMEJIPANGA KUBORESHA ELIMU NCHINI” – BASHUNGWA.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Prof. Joyce Ndalichako amesema Serikali imedhamiria kutoa fursa kwa vijana nchini ili waweze kuondokana na changamoto ya ajira.
Add a commentSerikali ya Tanzania na Japan zimesaini mikataba mitatu ya mkopo na msaada yenye thamani ya Yen za Japan bilioni 37.9 sawa na takriban shilingi bilioni 761.8 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ukarabati wa Bandari ya Kigoma, uboreshaji wa miundombinu ya maji Zanzibar na Ujenzi wa Barabara ya Arusha-Holili.
Add a commentWaziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Balozi, Dkt. Pindi Chana amewataka watumishi wa umma kufanya kazi kwa weledi, ufanisi na kuzingatia taratibu na kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria ili kutoa huduma bora kwa umma.
Add a commentRead more: WANAOFANYA KAZI KWA MAZOEA WAONYWA DHIDI YA TABIA HIYO.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amemteua aliyekuwa mwandishi wa BBC Zuhura Yunus Abdalla kuwa mkurugenzi wa mawasiliano ya rais.
Add a commentRead more: ZUHURA YUNUS ATEULIWA KUWA MKURUGENZI MAWASILIANO YA IKULU.
Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]
Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]
ROSATOM, taasisi ya nishati ya nyuklia ya serikali ya Urusi ambayo iliwaalika zaidi ya waandishi wa habari 15 kutoka nch [ ... ]
Copyright © 2023 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.