Star Tv

Jaji Mstaafu Mark Bomani ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa kwanza wa Tanzania, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 11, 2020, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Afisa Uhusiano wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha, amethibitisha na kusema kuwa Jaji Mstaafu Mzee Bomani alilazwa hospitalini hapo kwa siku 24.

"Jaji Mstaafu amefia hapa Muhimbili, amefariki majira ya saa 4:00 usiku wa kuamkia leo, na alikuwa hapa hospitalini kwa siku 24", amesema Aligaesha.

Jaji Mstaafu Mark Bomani alizaliwa 22 Oktoba 1943, Wete, Pemba-Zanzibar alikuwa ni mwanasheria mkuu kwa mwaka 1965 hadi 1976 wakati wa Utawala wa Rais wa Kwanza wa Tanzania, Julius Kambarage Nyerere.

Baada ya Jaji Bomani, alifuatiwa na Joseph Warioba na Jaji huyo amefariki akiwa ni Jaji mstaafu ambaye ana kampuni binafsi ya sheria.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.