Star Tv

Msemaji wa jeshi la Polisi nchini SACP David Misime amesema hali ya usalama na usimamizi wa ulinzi katika kampeni zinazoendelea nchini ni shwari na unaendelea vizuri.

Amesema Jeshi la Polisi limejiandaa vizuri katika kukabiliana na matishio ya aina yoyote ya kiusalama ambapo ulinzi umeimarishwa katika maeneo yote ya nchi ili kuhakikisha kampeni za uchaguzi mkuu zinafanyika kwa amani na utulivu.

Aidha, Kamanda Misime amewatahadharisha wananchi, viongozi wa kisiasa pamoja na wadau wengine wa uchaguzi kuendelea kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria za nchi.

Misime ametoa onyo kwa watu wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii na ikiwa itatokea baadhi ya watu wamefanya mambo yatakayopelekea uvunjifu wa amani na usalama wa nchi watawajibishwa ipasavyo.

Jeshi la Polisi limesema liko imara kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama nchini inaendelea kuwa shwari hususani katika kipindi hiki ambacho kampeni zinaendelea, Ambapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza Uchaguzi Mkuu kufanyika siku ya Jumatano Octoba 28, 2020.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.