Star Tv

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma inatarajiwa kuwafikisha mahakamani watu 10 katika mahakama za Dodoma na Bahi na kuwafungulia mashauri yanayohusiana na Rushwa akiwemo Mhadhiri Msaidizi Chuo kikuu cha Dodoma akihusihwa na rushwa ya ngono.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Agosti 13,2020 jijini Dodoma, Mkuu wa TAKUKURU mkoani humo Sosthenes Kibwengo amesema kwa kushirikiana na ofisi ya taifa ya mashtaka, watamfikisha mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma Bw.Jacob Paul Nyangusi [43]mhadhiri Msaidizi wa chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Baada ya kumfikisha mahakamani, watamfungulia shauri la uhujumu uchumi kwa kosa la kutaka rushwa ya ngono kinyume na kifungu cha 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11 /2007 ikisomwa pamoja na aya ya 21 jedwali la kwanza na vifungu vya 57(1)na 60(2) vya sheria ya uhujumu uchumi sura ya 200 marejeo ya mwaka 2020.

Bwana Kibwengo amefafanua kuwa,Majira ya saa 3 usiku wa tarehe 3,Oktoba,2018 TAKUKURU ilimkamata Bw.Nyangusi nyumbani kwake eneo la Nyumba Mia tatu jijini Dodoma muda mfupi kabla hajatekeleza nia yake ovu ya kufanya ngono na aliyekuwa mwanafunzi wake wa mwaka wa kwanza wa shahada ya sanaa katika jiografia na Mazingira.

Mkuu huyo wa TAKUKURU mkoani Dodoma,ameendelea kufafanua kuwa ,awali TAKUKURU ilipokea taarifa kuwa mtuhumiwa alimtaka mwanafunzi wake huyo kingono kama sharti la kumsaidia ili aweze kufanya mitihani ya marudio na kumwezesha kufaulu katika somo lake ,na ndipo ikaweka mtego na kumkamata.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.