Star Tv

Katika kuhakikisha kwamba tija ya uzalishaji wa mazao ya kilimo inaongezeka ili kujitosheleza kwa chakula na malighafi za viwandani, Wizara ya Kilimo imeendelea kuhamasisha matumizi ya mbolea ili kufikia kilo 50 za virutubisho kwa hekta moja kama ilivyopendekezwa na wakuu wa nchi za Afrika kupitia Azimio la Abuja la mwaka 2006.

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga ameeleza kuwa bei ya mbolea msimu wa 2020/21 imepungua kwa wastani wa shilingi 1,316 kwa mfuko wa kilo 50 wa UREA ikilinganishwa na msimu wa 2019/20, Na kwa upande wa DAP bei imepungua kwa wastani wa shilingi 2,860 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na msimu wa 2019/20.

Waziri Hasunga ameeleza hayo leo tarehe 11 Agosti 2020 ameyasema hayo wakati akitangaza bei mpya ya Mbolea kwa msimu wa mwaka 2020/2021 wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma.

Uingizaji wa mbolea kupitia BPS ambao unahusu mbolea za Urea, DAP, NPK, CAN na SA hivyo BPS umefanya gharama za usafirishaji wa mbolea baharini kushuka kwa kiasi kikubwa kutoka Tshs 23,000/= hadi Tshs 2,350/= Tshs kwa mfuko mmoja wa kilo 50.

Amesema kuwa pamoja na punguzo hilo la bei ya mbolea kwa msimu wa 2020/21 ukilinganisha na msimu wa 2019/20, vyama vya ushirika vilivyoshiriki zabuni ya BPS kwa msimu huu wa mwaka huu vitawauzia mbolea wanachama wao kwa bei nafuu zaidi ya bei elekezi inayotolewa na Serikali.

Waziri Hasunga amesema kuwa mbolea iliyoagizwa na vyama vya ushirika imewafikia wanachama wao mpaka vijijini walipo pasipo adha wala usumbufu wowote.

Aidha, kuhusu wastani wa bei ya mbolea ya DAP kitaifa kuanzia leo tarehe 11 Agosti 2020 kwa msimu wa 2020/21 itakuwa shilingi 55,573 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na shilingi 58,433 kwa mfuko wa kilo 50 msimu wa 2019/20.

Kwa upande wa mbolea ya UREA, wastani wa bei kitaifa kwa msimu wa 2020/21 itakuwa shilingi 48,070 kwa mfuko wa kilo 50 ikilinganishwa na shilingi 49,386 msimu wa 2019/20, huku waziri hasunga akifafanua mchanganuo wa bei elekezi za mbolea kutofautiana kimkoa ambapo amesema kuwa mbolea ya DAP na UREA kwa Mkoa mmoja na mwingine zinatofautiana kutokana na umbali kutoka Dar es Salaam, hali ya barabara na gharama za usafiri.

 

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.