Star Tv

Mchakato wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa kupata wagombea katika nafasi mbalimbali unaanza leo ambapo mikutano ya ngazi ya wilaya/majimbo itapiga kura za mapendekezo kati ya leo na kesho.

Upigaji wa kura unaoanza leo unahusisha kura za maoni za kuwapata wagombea katika nafasi za ubunge, uwakilishi, udiwani (Tanzania Bara) na usheha kwenye wadi visiwani Zanzibar.

Baada ya mikutano hiyo, Julai 30 kutakuwa na vikao vya kamati za siasa za majimbo kuwajadili wagombea na kutoa mapendekezo kwenye kamati za siasa za wilaya.

Vikao vya uteuzi kwa wagombea ubunge vitafanywa na Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu (NEC) ya CCM kwa Tanzania Bara na ujumbe wa Baraza la Wawakilishi ni Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar.

Latest News

Mgogoro wa Maji unatishia Amani Duniani, inasema ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa...
21 Mar 2024 14:18 - Kisali Shombe

Siku ya Maji Duniani ambayo inafanyika tarehe 22 Machi ikiwa na kaulimbiu: 'Maji kwa Ustawi na Amani. Ambapo maji ni moj [ ... ]

Matarajio katika mkutano wa BRICS nchini Afrika Kusini, Jumanne tarehe 22/2023
21 Aug 2023 12:14 - Kisali Shombe

Mkutano huo ambao utafanyikia Johannesburg nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne, tarehe 22 Agosti 2023, unatarajiwa kuhu [ ... ]

Rais Ramaphosa Kuwa Mwenyeji wa Rais Xi Jinping wa China
21 Aug 2023 11:11 - Kisali Shombe

Rais Cyril Ramaphosa Jumanne ya tarehe 22 Agosti 2023, atakuwa mwenyeji wa Mheshimiwa Rais Xi Jinping wa China katika Zi [ ... ]

Other Articles

Social Media

Copyright © 2024 . Star Tv - Tanzania. All Rights Reserved.