Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo , Zitto Kabwe na viongozi wengine saba wa Chama hicho wameripoti Kituo Kikuu cha Polisi Mkoani Lindi kama walivyohitajika.
Naibu Katibu wa Kamati ya Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo, Janeth Rithe wakati akitoa taarifa hiyo amesema viongozi hao wametakiwa kuripoti tena Polisi mkoani Lindi Julai 20, 2020.
Zitto pamoja na viongozi wengine akiwemo Mbunge wa Kilwa Kusini aliyemaliza muda wake, Suleiman Bungara walikamatwa na Polisi Wilayani Kilwa Juni 23, 2020 kwa kile ambacho Polisi walikiita ‘kuhatarisha amani’.